uchaguzi

Uchaguzi Tanzania
Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.

Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.

Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.

Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.

Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
  1. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Rais wa Madagascar ajiuzulu kuelekea kwenye uchaguzi wa Novemba 2023

    Rais wa Madagascar, Andry Rajoelina amejiuzulu baada tu ya kuthibitishwa rasmi kuwa mgombea katika uchaguzi wa Rais wa taifa hilo uliopangwa kufanyika Novemba 9, taarifa hii ni kwa mujibu wa mahakama ya kikatiba ya nchi hiyo. Katiba ya Madagaska inamtaka kiongozi mkuu wa nchi anayetaka kugombea...
  2. R

    JamiiForums Tanzania Mbatia: Tusiwekeze fedha zetu 125 bilioni kwenye uovu

    Mbatia ametoa rai kwa Rais samia /serikali kuwa isiwekeze shiling 125 billioni kuimarisha uovu, badala yake iziweke kwenye kuendeleza maisha ya watanzania. Ametoa mfano, zikiwekezwa Muhimbili, zitatoa huduma bora kwa watu wake! Serikali imetenga fedha hizo kununua silaha kudhibiti lolote...
  3. J

    JamiiForums Tanzania Chadema wakishiriki Uchaguzi kwa Tume hii ya Uchaguzi basi CCM itashinda kirahisi na Wasiposhiriki basi CCM itashinda kiubwete kabisa!

    Muundo wa sasa wa Tume ya Uchaguzi ni sawa na Mtego wa Panya hunaswa wahusika na wasiohusika Angalizo: Chadema wakishiriki Uchaguzi kwa Tume hii ya Uchaguzi ni Wazi CCM itashinda kirahisi lakini Wao Chadema watapata Wabunge na Madiwani Wawili Watatu Ikiwa Chadema hawatashiriki itakuwa ni...
  4. maganjwa

    JamiiForums Tanzania Je, kama hakuna Katiba Mpya wala Tume Huru kuna haja ya uchaguzi?

    Habari za humu ndani naamini ninyi ni wazima Mimi nauliza tu Maana kila moja anajua kitu gani kinakwenda kufanywa na ccm. Kwanini isianzishwe mikutano ya kudai mchakato wa katiba na tume ya Uchaguzi nchi nzima Maana mda umeisha sana mwakani ni Uchaguzi wa serikali za mitaa na 2025 uchaguzi...
  5. Mwande na Mndewa

    JamiiForums Tanzania Group Jipya la wana-CCM kuelekea uchaguzi ujao, watu wamechafukwa

    Dr Kesho: Naomba kutoa Shukrani kuniunga Huku ila kwasasa sihitaji kuwa magroup yoyote ya Kisiasa Wala kijamii Sitaki Siasa. Mwenyekiti aliyepita: Samahani ndugu zangu, Mie siyo mwanachama wa CCM hivyo sina sababu ya kuwepo humu kwenye mambo ya CCM yenu. Katibu tawi: Sas mimi kwa upande wangu...
  6. B

    JamiiForums Tanzania Ombi: Rais Samia harakisha mchakato wa Katiba Mpya na Tume Huru

    Kila nikitazama jinsi Mchakato wa Katiba Mpya na Tume huru ya uchaguzi inavyosua sua huku muda bado upo nashangaa sana.. Dkt. Samia Suluhu Hassani ni mpenda haki na juu ya yote ni Mwislam anayetii Mafundisho ya Mtume Muhamad Mtume wa Mwenyezi Mungu. Je, kusua sua kwa jambo hili ndio kusema...
  7. T

    JamiiForums Tanzania Kuna uwezekano mkubwa Uchaguzi Mkuu 2025 zaidi ya wabunge 20 wa CCM wakapita bila kupingwa. Niko pale nakula popcorn

    Huu ni mtazamo wangu binafsi kuhusu hali ya kisasa nchini sijui ni nini kimetokea kwenye taifa letu. Hilo jambo litatokea si Kwa sababu watu wanamapenzi mema na CCM na wala si kwa sababu watu wana Imani na CCM na sera zake, bali itatokea Kwa sababu ya watanzania kukosa mwamko wa kisiasa...
  8. G-Mdadisi

    JamiiForums Tanzania TAMWA ZNZ, MCT, wadau wa Habari watoa tamko Mjumbe Tume ya Uchaguzi Zanzibar kuzuiwa kuzungumza baada ya Kuapishwa na Rais Mwinyi

    CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA Zanzibar), Baraza la Habari Tanzania (MCT), Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo Zanzibar (WAHAMAZA), pamoja na Klabu ya Waandishi wa Habari Zanzibar (ZPC), zikishirikiana na Kamati ya Wataalamu wa masuala ya habari Zanzibar (ZAMECO)...
  9. B

    JamiiForums Tanzania Kushindwa uchaguzi ni pamoja na kuibiwa kura, kulikoni kulia lia

    Penye ukweli pasi na kujali kambi ni heri kuusema. Vinginevyo tutaendelea kutwanga maji kwenye kinu milele. Hongereni CCM Kwa kushinda chaguzi zenu na kama mabwege yakiendelea kulaza damu kazeni uzi hapo hapo. Kwani malengo ya chama cha siasa nini? Si walisema "the end justifies the means?"...
  10. T

    JamiiForums Tanzania Natafuta viashiria muhimu vya CCM kuanguka uchaguzi unaokuja na upinzani kushinda sivioni

    Kama mada inavyojieleza hapo juu na kama waswahili wasemavyo wa kushiba huonekana mezani, awamu hii tofauti sana na hali ilivyokuwa kuelekea uchaguzi wa mwaka 2015, sijaona viashiria vingi muhimu vinavyotoa matumaini ya ccm kuanguka katika uchaguzi unaokuja. Mwaka 2015 kulikuwa na vuguvugu...
  11. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Zimbabwe: Upinzani waitisha Maandamano Nchi nzima kupinga Matokeo ya Uchaguzi

    Kiongozi cha Chama Kikuu cha Upinzani cha Citizens Coalition for Change (CCC), kimetangaza kuchuka hatua hiyo kwa maelezo kuwa Matokeo ya Uchaguzi Mkuu yaliyompa Ushindi Rais Emmerson Mnangagwa ni Batili. Maandamano hayo yatafanyika katika Majimbo 10 huku CCC ikiwaomba Wanaharakati kusambaza...
  12. R

    JamiiForums Tanzania Serikali ina la kuwaambia wananchi juu ya kutokupatikana kwa mtandao kipindi cha Uchaguzi 2020?

    Mmoja wa washiriki kwenye Kongamano la Maendeleo ya Sekta ya Habari 2020 amerusha swali kwa wawasilishaji Mike Mushi na Ayoub Rioba pamoja na meza ya Mgeni Rasmi Waziri Nape Nnauye kwanini serikali haijatoa ufafanuzi juu ya kupotea kwa internet kipindi cha uchaguzi mwaka 2020 kama serikali hivi...
  13. peno hasegawa

    JamiiForums Tanzania Tanzania bila Maandamano hakuna Katiba mpya kabla ya Uchaguzi Mkuu 2025

    Nimeandika kwa kifupi , nitachangia nikiamka.
  14. S

    JamiiForums Tanzania CHADEMA msilete longolongo - Dai dume ni KATIBA mpya na Tume Mpya ya Uchaguzi

    Nina wasiwasi na hawa CHADEMA kuwa ni tawi la CCM ,ukiangalia kwa undani utaona wananchi tumehamishiwa kwenye bandari,mbuga na mambo mengi ambayo mwisho wa siku tunapigwa na kufungwa bao la kisigino. Bila ya madai dume ya kudai katiba mpya na tume mpya iliyo huru ya uchaguzi itakuwa haya...
  15. B

    JamiiForums Tanzania Tudai uchaguzi wa haki badala ya kudai kuibiwa baada ya chaguzi

    Zimbabwe tayari wapinzani wanadai kuibiwa uchaguzi. Gabon uchaguzi wao ni leo: "Huko kwenye mtandao wa internet, TCRA ya huko tayari imeshafanya yake." Zaidi mno Serikali ya huko imepiga marufuku uwepo wa waangalizi na wanabari wa kimataifa. 1. Twendeni mahakamani, 2. Kampeni zetu ziwe na...
  16. B

    JamiiForums Tanzania Uchaguzi Zimbabwe, upinzani Tanzania bado hatujifunzi?

    Uchaguzi wa karibuni kwenye mazingira kama yetu, ni huu wa juzi Zimbabwe. Waangalizi mbali mbali mbali wakiwamo SADC, Carter Center na wengine, wamelazimika kuuita kwa majina yake. Yaani kwa ufupi, wameuona siyo uchaguzi bali ni wizi wa mchana kweupe. Hapa chini ni sampuli za yale matokeo...
  17. BARD AI

    JamiiForums Tanzania Waangalizi wa Umoja wa Ulaya wadai Uchaguzi wa Zimbabwe sio Huru na Haki

    Kupitia ripoti yao, Waangalizi kutoka Ujumbe wa Umoja wa Ulaya (EU EOM) wamesema Uchaguzi huo ulikuwa na Uminyaji wa Haki, Ukosefu wa Fursa Sawa na Mazingira Magumu kwa Wapiga Kura. EU EOM imeongeza kuwa kulikuwa na ukamataji wa kutumia nguvu wa Waangalizi 39 wa Mashirika ya Kiraia ambao...
  18. GENTAMYCINE

    JamiiForums Tanzania Kama Uchaguzi wao umetawaliwa na Rushwa kwa 85% wanapata wapi uhalali wa Kupingana na Tamko la Werevu TEC?

    Na bahati nzuri Wanaosema kuwa Uchaguzi wenu wa Jana ulijaa Rushwa tupu ni Wenzenu ( tena baadhi yao ) ni Wapiga Kura mnapata wapi Uthubutu wa Kuukana na Kuukosoa Msimamo wa wenye Akili Kubwa duniani TEC na Kanisa Katoliki ( GENTAMYCINE nikiwemo ) juu ya Sakata la Uwekezaji wa DP World na...
  19. Azniv Protingas

    JamiiForums Tanzania UTEUZI: Rais wa Zanzibar amemteua Jaji George Joseph kazi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi

    Jaji George Joseph Kazi ameteuliwa leo na Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe.Dk.Hussein Ali Mwinyi kuwa Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar ataapishwa tarehe 28 Agosti, 2023 saa 8 Mchana Ikulu Zanzibar na wajumbe wa Tume hiyo. Uteuzi wake unaanza leo 24 Agosti, 2023...
  20. Roving Journalist

    JamiiForums Tanzania Rais Mwinyi mgeni rasmi katika Mjadala wa Demokrasia kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa, Vijiji na Vitongoji 2024 na Uchaguzi Mkuu 2025

    Mkutano wa kitaifa wa wadau kujadili hali ya demokrasia nchini kuelekea uchaguzi mkuu wa serikali za mitaa, vijiji na vitongoji 2024 na uchaguzi mkuu 2025 Mkutano huu ni wa siku mbili, kusoma yaliyojiri siku ya kwanza bofya viunga hivi 1. Mkutano wa Kitaifa wa wadau wa Demokrasia: AveMaria...
Back
Top Bottom