Uchaguzi hasa wa viongozi katika nchi ni utaratibu (mchakato) rasmi unaoendeshwa kwa mujibu wa sheria kuwawezesha wananchi kufanya maamuzi kwa njia ya kuwapigia kura kuwachagua watu ambao wanawataka kuwaongoza kwa kipindi maalum.
Uchaguzi ni utaratibu wa kawaida wa demokrasia wa kuwapata wawakilishi wa kisiasa ambao umekuwa ukitumika tangu karne ya 17. Kuna aina tatu za msingi za uchaguzi zinazotumiwa kuwapata viongozi kulingana na mfumo unaotumiwa na nchi husika.
Aina hizo ni uchaguzi wa Rais, Uchaguzi wa Wabunge na Wawakilishi katika Baraza la Kutunga Sheria na Uchaguzi wa Viongozi wa Serikali za Mitaa.
Vyama vya Siasa kwa upande wao navyo huendesha chaguzi ambazo zinajulikana kwa jina la “Chaguzi wa Msingi” zinazotumika kuwachagua wateuliwa wa vyama katika aina za uchaguzi ambazo zimetajwa hapo juu.
Endapo Tume haitaridhika kabla ya kutangaza matokeo ya uchaguzi kwamba kulikuwa na kutokufuatwa kwa taratibu, matumizi mabaya au ukiukwaji wa taratibu za uchaguzi au pale ambapo kura za wagombea waliopata kura za juu imelingana, Tume itasimamisha au kufuta uchaguzi au sehemu yoyote ya uchaguzi na itatangaza siku nyengine ya kurudiwa kwa uchaguzi huo.
Sasa hivi wanajipitisha pitisha eti wanasikiliza kero.
Kero gani ambazo hujaziona na kuzifanyia kazi miaka mitano yoote ambazo utatatua kwa miezi michache iliyobaki.
Sijaona watu wanafiki kama hawa.
Eti wako madarakani miaka 60 ya Uhuru leo ndio wanajifanya hawajui kama Wanachi wana Maji...
Taarifa ikufikie popote ulipo kwamba , leo 09/02/2024 kuna Uchaguzi wa Viongozi wa Chadema Mbeya Mjini .
Habari zinadokeza kwamba Ni kama vile Mbeya Mjini leo ni siku ya Mapumziko , huku wafanyakazi wa Serikali na makampuni wakitoroka makazini mapema , kwa kisingizio cha ibada ya Ijumaa ...
https://www.youtube.com/watch?v=st-YFWzMvWQ
RAIS SAMIA: UCHAGUZI UTAKUWA HURU NA WA HAKI
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amesema haki, demokrasia, sheria na utawala bora utadumishwa kwa watu wote wakati wa Uchaguzi wa Serikali za Mitaa unaotarajiwa kufanyika...
SENEGAL: Wabunge wa chama Tawala na wengine wanaounga mkono Serikali, wamepiga Kura na kupitisha ombi la Rais Macky Sall, la kuahirisha Uchaguzi Mkuu uliopangwa kufanyika Februari 25, 2024 ambapo sasa umesogezwa mbele hadi Desemba 15, 2024 .
Hatua hiyo imefikiwa baada ya Wabunge wa upinzani...
Bunge limepitisha mswada uliopelekwa bungeni na serikali kufanya mabadiliko ya katiba kwenye kipengele cha tume ya uchanguzi.
Sasa kwa sheria mpya iliyopitishwa na bunge wakurugenzi wa wilaya na mamea wataacha kuwa wasimamizi wa uchaguzi moja kwa moja kutokana na nafasi zao wilayani. Badala...
Hili jamaa linalo ongoza Senegal lina sababu gani za msingi kuhairisha uchaguzi ? Au ndio upuuzi wa kung'ang'ania madaraka kama kawaida ya maviongozi ya Afrika ?
Hivi hivi Senegal inaweza kuingia kwenye machafuko ya wenyewe kwa wenyewe halafu baadae lawama anaanza kupewa marekani na ulaya...
https://youtube.com/shorts/Q-lZqr4sOQM?si=tYeBkv32gKrQKx0-
CCM haya ndiyo yanayokuja acheni kuliteka Taifa letu kwa MASLAHI yenu wachache.
CHADEMA PEOPLE'S POWEER!!!✌️✌️✌️🤞
04 February 2024
Dakar, Senegal
RAIS WA SENEGAL AFANYA MAPINDUZI YA 'KIKATIBA' KWA KUFUTA UCHAGUZI MKUU
Rais wa nchi tulivu iliyokwepa Mapinduzi ya kijeshi ya Africa Magharibi ya Senegal imeigia katika mtihani mkubwa toka ipate uhuru wake. Hii ni mara ya kwanza katika historia ya nchi hiyo...
Abdulrahman Kinana amesema Uchaguzi ujao utakuwa wa haki kwani wasimamizi watakuwa Waadilifu na Waaminifu.
"Bunge limekubali (Bunge la Tanzania) limesema wasimamizi wa uchaguzi watakuwa watumishi wa umma waandamizi. Mtu atateuliwa kwa sifa; sifa za uadilifu, uhodari wa kazi na uaminifu...
Nimefuatilia mijadala Bungeni kuhusu Sheria za Uchaguzi. Nilitegemea kusikia ushauri, maoni yaliyotolewa na wadau wote yakijadiliwa moja baada ya moja lakini cha kushangaza Wabunge wengi wamejikita kujadili tu marekebisho kuhusu Wakurugenzi na Jinsia.
Kuna ushauri uliotolewa na wadau kama...
Tusidanganywe na lugha zenye hadaa nyingi za wabunge wetu wanaojadili miswada ya sheria za Uchaguzi. Hawana nia njema kwa nchi
Hawana maono mema kwa nchi
Hawana huruma kwa nchi.
Kinachojulikana sasa ni kwamba, Serikali na Chama cha Mapinduzi ni wamoja dhidi ya uhalali, haki na wajibu kwa...
Moja ya malalamiko makubwa kabisa ya chama kikuu cha upinzani nchini cha Chadema na wananchi walio wengi nchini, ni kukosoa suala la wakurugenzi wa miji kuwa wasimamizi wa uchaguzi Mkuu.
Ni jambo lililo wazi kuwa katika suala zito sana la uchaguzi Mkuu, ni lazima wanaopangwa kusimamia uchaguzi...
Mbombo ngafu, hii imekaaje?
CHADEMA hawawatambui Halima Mdee na wenzake, lakini wanaenda kwenye kamati ya Bunge la akina Mdee kutoa maoni yao kuhusu sheria za uchaguzi, na wanatarajia hao hao wawapitishie sheria tamu na nzuri ambazo zitawafanya waanze kula, na wanaokula sasa wakubali kwa hiyari...
Mbunge wa jimbo la Kiteto ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria Edward Olelekaita amesema Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania haikubainisha Tume ya Uchaguzi iitwe jina gani, hivyo hakuna tatizo katika kubadili jina la sasa ambalo ni Tume ya Taifa...
Habari JF , kwa kifupi kabisa kwa katiba tuliyo nayo ni katiba ambayo ina upendeleo mkubwa kwa watawala na kuwapa nguvu kubwa kutawala .
Kwa maana nyingine sio katiba ya kizalendo sababu haiwapi nguvu sana wananchi na hailindi sana mali za Nchi yetu .
Chama chochote kikisha ingia madarakani...
Wakuu,
Msikilize kiongozi huyu aliye ambiwa amkaribishe Makonda, yaani ni kampeni kabisa zimeanza.
"Wilaya ya Hai sasa imepata maendeleo makubwa, ninachotaka kuwaomba msifanye makosa, kina mama na akina baba twendeni na Dr. Samia Suluhu Hassan.
"Tunakwenda kwenye uchaguzi mwaka kesho...
Wakuu,
Huwa unazingatia nini kabla hujaamua kwenda kwenye mkutano wa siasa, iwe mkutano wa hadhara au kampeni? Ni mada inayoenda kuzungumzwa, mzungumzaji mwenyewe, nguvu ya chama au nini?
Nini huwa na umuhimu zaidi kwako ambapo kisipokuwepo huwezi kwenda kwenye mkutano huo au hata kuufatilia...
Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Utawala, Katiba na Sheria, Dkt. Joseph Mhagama amesema maandamano sio suluhu ya kupata muafaka wa maoni ya Muswada wa Sheria ya Uchaguzi na kuongeza kuwa tayari maoni hayo yameshapokelewa na kupelekwa Bungeni na kamati yake inaendelea kuyachakata...
Wakuu kwema?
Kama kichwa kinavyosema hapo juu, kauli gani imewahi kutolewa na mwanasiasa iwe kwenye kampeni, mkutano wa hadhara, au kiongozi akiwa anatimiza majukumu yake ikakufanya uchukie siasa ama uache kabisa kufatilia mambo yanayohusu siasa?
"Haiwezekani Mkurugenzi nikuteue mimi...
JamiiForums uses cookies to help personalise content, tailor your experience and to keep you logged in if you register.
By continuing to use this site, you are consenting to our use of cookies.